Kanisa la Moravian Tanzania – Jimbo la Kusini ni kanisa la Kikristo la Kiprotestanti, lilianzishwa mnamo karne ya 19 na wamisionari kutoka Herrnhut, Ujerumani ambao walifika Tanzania na kuanza kufanya kazi katika Mkoa wa Mbeya-Rugwe mwaka 1891.
Hii ilikuwa matokeo ya upanuzi wa umisionari wa Waprotestanti ambao walianzisha kanisa huko Kunward, Bohemia katika Jamhuri ya sasa ya Ucheki ‘Czech’ mwaka 1457. Kanisa lilienea katika Moravia, ambako lilipata jina lake, na kwa miaka mingi, liko sehemu nyingi duniani. MCT - SP ni mwanachama wa Baraza la Makanisa nchini Tanzania (CCT) na kutambuliwa kikamilifu na bodi ya umoja ya Moravian ulimwenguni (Unitas Fratrum).
Kanisa lina muundo ambao huenda hadi ngazi za chini hivyo, kuwezesha kuwa taasisi ya kuaminika zaidi na kuleta mabadiliko makubwa katika jamii. MCT-SP inashughulikia eneo la kusini mwa Tanzania na wilaya za Kyela, Rungwe na Ileje zenye idadi ya Wakristo zaidi ya 150'000 na imeongeza utumishi wake na kufikia eneo moja la umisioni Ruvuma na Njombe. Inaongozwa na Bodi ya watendaji ambao ni Askofu, Mwenyekiti, Makamu Mwenyekiti, Katibu Mkuu na Mweka hazina mkuu na ina ofisi kadhaa za idara zinazoshughulika na masuala ya kila siku, kuanzia kiroho hadi maendeleo ya kijamii na kiuchumi. https://www.mctsp.org
common.swipe_images
- Barua Pepe
- jk@moravianchurch.or.tz
- Simu
- 0732950091
- Anwani
- P.O.BOX 32 TUKUYU-MBEYA
- Mkoa
- Mbeya
- Wilaya
- Rungwe
- Kata
- Rungwe